Safarini Kigali!
Ndugu Wadadisi wa blogu hii kesho naelekea Kigali na Butare, Rwanda kwenda kujumuika, kuhuishwa na kudadisi. Kwa muda mrefu nimekuwa sana na hamu ya kuiona nchi hii ambayo ilijikita kwenye fikra zetu kwa namna ya pekee katikati ya miaka ya 90. Ni matumaini yangu kuwa nitapata mengi ya kusimulia kwenye blogu hii nikiwa huko au, Inshallah, nitakaporejea kutoka huko. Jalia na awabariki na kuwavusha salama salimini kuelekea mwaka mpya. Amen!

0 comments:
Post a Comment