Ihefu hadi Ikwiriri: Majuto ni Mjukuu?
TUTASHUGHULIKIA MATOKEO TU HADI LINI?
Sijasoma yote yaliyoandikwa katika mjadala huu wa Wanabidii lakini nina machache ya kuchangia kuhusu suala la Ikwiriri kwa kuwa ni eneo ambalo nimekuwa nikifanya kazi za utafiti kwa muda mrefu sasa.
Takriban miaka mitano mpaka kumi iliyopita hakukuwa na mfugaji wa ng'ombe hata mmoja. Wengi wa wafugaji ni wa kabila la wasukuma ambao wamehamia toka Ihefu. Tukumbuke serikali iliwafukuza/kuwahamisha Ihefu kinyume cha taratibu na kuwanyang'anya mifugo baadhi yao waliochelewa kuondoka. Walitakiwa kwenda maeneo tengefu ya Lindi na Mtwara na kwingineko. Maeneo tengefu mengi hayafai kwa ufugaji kwani hayakutengwa kwa kuzingatia mahitaji ya wafugaji: maji, malisho na huduma za kijamii. Hivyo wafugaji wamelazimika kubuni mbinu zao za kuweza ku-survive in the absence of effective structural, infrastructural and institutional support systems from the State.
Hali ikoje: Kwa kuwa hakuna kanuni nzuri za kuhakikisha kuishi kwa pamoja baina ya wakulima na wafugaji na kwa kuwa shughuli zao haziendani, kwa maana ya kwamba wanyama wa wafugaji wanaharibu mazao ya wakulima, hitilafu zilipotokea, wananchi (wakulima na wafugaji) walikimbilia ofisi za serikali za vijiji na polisi kuweza kupata usuluhishi. Kesi ziliongezeka mno. Polisi wetu na viongozi wetu wa vijiji, kata, tarafa na wilaya tunafahamu kuwa hawalipwi vizuri na serikali. Wafugaji ambao huwa wana uwezo bora kimaisha na kifedha kuliko wakulima katika maeneo ya Ikwiriri walianzisha mchezo mchafu wa kuhonga polisi na kuwabambikia kesi wakulima kuwa wao ndio wavurugao amani.
Nina mifano kadhaa kutoka kwa wananchi wengi niliopata kuongea nao. Mfano: Mzee XX amekuta mifugo shambani kwake na kuanza kujibizana na mfugaji YY kufikia hatua ya kutaka kupigana. Mkulima XX anatamka kuwa ni lazima suala hili alifikishe kunakohusika. Mfugaji YY anachukua pikipiki na kuwahi Ikwiriri police post. Mkulima XX anafika polisi, anakamatwa kuwa ametishia uhai wa Mfugaji YY na mifugo yake. Anawekwa ndani kwa muda ambao polisi wameamua wenyewe.
Nikitumia taarifa halisi ambazo si rasmi kwa kuwa hazijatolewa na vyombo vya usalama (polisi) lakini nimezipata toka kwa jamaa zangu waishio Ikwiriri:
Mapigano ya juzi ni kilele cha ugomvi ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka kadhaa sasa na wakulima ndio wamekuwa waathirika wakubwa. Huyu Mzee alieuawa Ijumaa aliwahi kutoa taarifa kuhusu wafugaji kuingiza mifugo shambani kwake mwaka jana. Alikamatwa na kuwekwa ndani. Alipotoka aliendelea kudai haki yake kwa kwenda mahakamani. Alishinda kesi mahakamani na mfugaji mhusika alitakiwa kuondosha mifugo yake mara moja. Lakini hakufanya hivyo kwa kuwa mahakama si yenye kusimamia migogoro ya wakulima na wafugaji on a daily basis but ni polisi, hivyo mfugaji aliendelea kuhonga polisi.
Siku ya tukio, mkulima mzee wa miaka 60 alikuta mifugo shambani kwake na kuanza kujibizana na wenye mifugo. Wafugaji walipiga kelele na kuchukua marungu, mapanga na silaha nyinginezo wakampiga mpaka kumuua yule mzee. Ina lillah wa in illaih rajiun! Wananchi wakaenda kutoa taarifa polisi Ikwiriri. Kwa mujibu wa wananchi, hawakupendezwa na namna polisi walivyolishughulikia suala hili. Waliona kuwa polisi wamechukulia kana kwamba kimekufa kiji-mnyama tu kidogodogo na si binadamu tena wa miaka 60 ambaye alishinda kesi mahakamani kuhusu mgogoro uliopelekea mauti yake. Wananchi wakulima wakasema "enough is enough".
Wakazifunga barabara za kutoka Lindi na Dar na kuanza kushambuliana na wafugaji. Kwa kuwa wafugaji waliompiga na kumuua yule mzee ni wa kabila la kisukuma, wakulima walilenga kuwashambulia wasukuma irrespective ya kuwa ni wafugaji ama la. Maduka, magari, nyumba na mali nyinginezo zinazomilikiwa na wasukuma zimechomwa moto. Polisi mmoja wa kabila la kisukuma amechomewa nyumba yake kubwa yenye wapangaji kadhaa kwani wananchi walimtuhumu kuwa huwa anawasaidia wasukuma wenzake.
Wakulima wa Ikwiriri nilioongea nao kwa simu wanahoji kwamba: kwa nini vyombo vya habari na jeshi la polisi wametoa takwimu za wafugaji waliojeruhiwa na kuharibiwa mali zao lakini hawajasema kuhusu WANANCHI WAKULIMA WA KABILA LA WANDENGEREKO WAWILI WALIOUAWA KWA RISASI NA MFUGAJI WA KABILA LA KISUKUMA SIKU YA MACHAFUKO? Kwao wao, wanadai kuwa hii bado inalenga kumkandamiza mkulima hasa wa kabila la kindengereko (nimetaja makabila kwa kuwa wao walioniambia wamesisitiza katika maandiko nifanye hivyo ili ichangie kuonesha ukandamizaji wa kabila la wandengereko. Mimi si mndengereko wa silazimishwi kufanya wanavyotaka wao, bali nimeona nifanye hivi kujibu hoja ya mmoja wa wachangiaji aliyehoji kwa nini ukabila umekuwa "issue" katika suala hili.)
Sasa hivi hali bado ni mbaya kwani Wandengereko wamedai hawawezi kuendelea kuishi kwa kuonewa na wasukuma, hivyo wasukuma waondoke. Hii ndio hali halisi kwa vyanzo nilivyoweza kuvifikia mimi. Maswali ambayo yameulizwa kuwa wafugaji waende wapi na ni nani mwenye haki zaidi ya ardhi, mkulima au mfugaji? Majibu yangu ni kama ifuatavyo:
Serikali ilipaswa itambue mahitaji ya wafugaji kama vile kutenga maeneo yenye malisho na maji ya kutosha na kuweka miundombinu ya kukidhi mahitaji hayo. Namna ambavyo serikali inaachia suala hili liwe baina ya wakulima na wafugaji ndicho chanzo kikubwa cha migogoro. Vijiji vingi vya Ikwiriri, Lindi na Mtwara vimeshurutishwa na serikali kutengeneza mipango ya matumizi bora ya ardhi ikiwemo kutenga maeneo ya wafugaji. Wananchi hawa hawana uzoefu na ufugaji na hivyo hawajui mahitaji maalum ya wafugaji. Kwa mfano, katika Kijiji cha Mavuji wilayani Kilwa, wananchi wametenga eneo la malisho ambalo liko milimani ambao mifugo haiwezi kutembea kwa urahisi. Mipango hii ya matumizi bora ya ardhi imetengenezwa bila ushiriki wa wafugaji kwa kuwa hakukuwa na wafugaji katika vijiji husika. Halmashauri za Wilaya husika zilikuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa mipango ya matumizi ya ardhi iliyotengenezwa imekidhi vigezo vya kitaalam ili kuepusha migogoro kama hii tunayoiona sasa. Kwa hali ilivyo sasa, tutegemee migogoro mingi kama hii kuibuka.
Tutaendelea kushughulikia matokeo mpaka lini ilihali vyanzo twavijua?
Mwandishi: Baruani Mshale
Sijasoma yote yaliyoandikwa katika mjadala huu wa Wanabidii lakini nina machache ya kuchangia kuhusu suala la Ikwiriri kwa kuwa ni eneo ambalo nimekuwa nikifanya kazi za utafiti kwa muda mrefu sasa.
Takriban miaka mitano mpaka kumi iliyopita hakukuwa na mfugaji wa ng'ombe hata mmoja. Wengi wa wafugaji ni wa kabila la wasukuma ambao wamehamia toka Ihefu. Tukumbuke serikali iliwafukuza/kuwahamisha Ihefu kinyume cha taratibu na kuwanyang'anya mifugo baadhi yao waliochelewa kuondoka. Walitakiwa kwenda maeneo tengefu ya Lindi na Mtwara na kwingineko. Maeneo tengefu mengi hayafai kwa ufugaji kwani hayakutengwa kwa kuzingatia mahitaji ya wafugaji: maji, malisho na huduma za kijamii. Hivyo wafugaji wamelazimika kubuni mbinu zao za kuweza ku-survive in the absence of effective structural, infrastructural and institutional support systems from the State.
Hali ikoje: Kwa kuwa hakuna kanuni nzuri za kuhakikisha kuishi kwa pamoja baina ya wakulima na wafugaji na kwa kuwa shughuli zao haziendani, kwa maana ya kwamba wanyama wa wafugaji wanaharibu mazao ya wakulima, hitilafu zilipotokea, wananchi (wakulima na wafugaji) walikimbilia ofisi za serikali za vijiji na polisi kuweza kupata usuluhishi. Kesi ziliongezeka mno. Polisi wetu na viongozi wetu wa vijiji, kata, tarafa na wilaya tunafahamu kuwa hawalipwi vizuri na serikali. Wafugaji ambao huwa wana uwezo bora kimaisha na kifedha kuliko wakulima katika maeneo ya Ikwiriri walianzisha mchezo mchafu wa kuhonga polisi na kuwabambikia kesi wakulima kuwa wao ndio wavurugao amani.
Nina mifano kadhaa kutoka kwa wananchi wengi niliopata kuongea nao. Mfano: Mzee XX amekuta mifugo shambani kwake na kuanza kujibizana na mfugaji YY kufikia hatua ya kutaka kupigana. Mkulima XX anatamka kuwa ni lazima suala hili alifikishe kunakohusika. Mfugaji YY anachukua pikipiki na kuwahi Ikwiriri police post. Mkulima XX anafika polisi, anakamatwa kuwa ametishia uhai wa Mfugaji YY na mifugo yake. Anawekwa ndani kwa muda ambao polisi wameamua wenyewe.
Nikitumia taarifa halisi ambazo si rasmi kwa kuwa hazijatolewa na vyombo vya usalama (polisi) lakini nimezipata toka kwa jamaa zangu waishio Ikwiriri:
Mapigano ya juzi ni kilele cha ugomvi ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka kadhaa sasa na wakulima ndio wamekuwa waathirika wakubwa. Huyu Mzee alieuawa Ijumaa aliwahi kutoa taarifa kuhusu wafugaji kuingiza mifugo shambani kwake mwaka jana. Alikamatwa na kuwekwa ndani. Alipotoka aliendelea kudai haki yake kwa kwenda mahakamani. Alishinda kesi mahakamani na mfugaji mhusika alitakiwa kuondosha mifugo yake mara moja. Lakini hakufanya hivyo kwa kuwa mahakama si yenye kusimamia migogoro ya wakulima na wafugaji on a daily basis but ni polisi, hivyo mfugaji aliendelea kuhonga polisi.
Siku ya tukio, mkulima mzee wa miaka 60 alikuta mifugo shambani kwake na kuanza kujibizana na wenye mifugo. Wafugaji walipiga kelele na kuchukua marungu, mapanga na silaha nyinginezo wakampiga mpaka kumuua yule mzee. Ina lillah wa in illaih rajiun! Wananchi wakaenda kutoa taarifa polisi Ikwiriri. Kwa mujibu wa wananchi, hawakupendezwa na namna polisi walivyolishughulikia suala hili. Waliona kuwa polisi wamechukulia kana kwamba kimekufa kiji-mnyama tu kidogodogo na si binadamu tena wa miaka 60 ambaye alishinda kesi mahakamani kuhusu mgogoro uliopelekea mauti yake. Wananchi wakulima wakasema "enough is enough".
Wakazifunga barabara za kutoka Lindi na Dar na kuanza kushambuliana na wafugaji. Kwa kuwa wafugaji waliompiga na kumuua yule mzee ni wa kabila la kisukuma, wakulima walilenga kuwashambulia wasukuma irrespective ya kuwa ni wafugaji ama la. Maduka, magari, nyumba na mali nyinginezo zinazomilikiwa na wasukuma zimechomwa moto. Polisi mmoja wa kabila la kisukuma amechomewa nyumba yake kubwa yenye wapangaji kadhaa kwani wananchi walimtuhumu kuwa huwa anawasaidia wasukuma wenzake.
Wakulima wa Ikwiriri nilioongea nao kwa simu wanahoji kwamba: kwa nini vyombo vya habari na jeshi la polisi wametoa takwimu za wafugaji waliojeruhiwa na kuharibiwa mali zao lakini hawajasema kuhusu WANANCHI WAKULIMA WA KABILA LA WANDENGEREKO WAWILI WALIOUAWA KWA RISASI NA MFUGAJI WA KABILA LA KISUKUMA SIKU YA MACHAFUKO? Kwao wao, wanadai kuwa hii bado inalenga kumkandamiza mkulima hasa wa kabila la kindengereko (nimetaja makabila kwa kuwa wao walioniambia wamesisitiza katika maandiko nifanye hivyo ili ichangie kuonesha ukandamizaji wa kabila la wandengereko. Mimi si mndengereko wa silazimishwi kufanya wanavyotaka wao, bali nimeona nifanye hivi kujibu hoja ya mmoja wa wachangiaji aliyehoji kwa nini ukabila umekuwa "issue" katika suala hili.)
Sasa hivi hali bado ni mbaya kwani Wandengereko wamedai hawawezi kuendelea kuishi kwa kuonewa na wasukuma, hivyo wasukuma waondoke. Hii ndio hali halisi kwa vyanzo nilivyoweza kuvifikia mimi. Maswali ambayo yameulizwa kuwa wafugaji waende wapi na ni nani mwenye haki zaidi ya ardhi, mkulima au mfugaji? Majibu yangu ni kama ifuatavyo:
Serikali ilipaswa itambue mahitaji ya wafugaji kama vile kutenga maeneo yenye malisho na maji ya kutosha na kuweka miundombinu ya kukidhi mahitaji hayo. Namna ambavyo serikali inaachia suala hili liwe baina ya wakulima na wafugaji ndicho chanzo kikubwa cha migogoro. Vijiji vingi vya Ikwiriri, Lindi na Mtwara vimeshurutishwa na serikali kutengeneza mipango ya matumizi bora ya ardhi ikiwemo kutenga maeneo ya wafugaji. Wananchi hawa hawana uzoefu na ufugaji na hivyo hawajui mahitaji maalum ya wafugaji. Kwa mfano, katika Kijiji cha Mavuji wilayani Kilwa, wananchi wametenga eneo la malisho ambalo liko milimani ambao mifugo haiwezi kutembea kwa urahisi. Mipango hii ya matumizi bora ya ardhi imetengenezwa bila ushiriki wa wafugaji kwa kuwa hakukuwa na wafugaji katika vijiji husika. Halmashauri za Wilaya husika zilikuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa mipango ya matumizi ya ardhi iliyotengenezwa imekidhi vigezo vya kitaalam ili kuepusha migogoro kama hii tunayoiona sasa. Kwa hali ilivyo sasa, tutegemee migogoro mingi kama hii kuibuka.
Tutaendelea kushughulikia matokeo mpaka lini ilihali vyanzo twavijua?
Mwandishi: Baruani Mshale


0 comments:
Post a Comment